Kufungamanisha Sekta ya Viwanda na Sekta ya Kilimo
Mheshimiwa Spika, adhma ya nchi yetu kuwa ya Viwanda ni adhma yetu sote. Jambo hili ni jambo la Maendeleo na halina ushabiki wa kivyama. Tumepitisha Mpango wa Maendeleo katika Bunge hili na kwa hiyo ni Mpango wa Nchi sio mpango wa vyama tena. Hivyo sote kwa pamoja tunafanya kazi ya kuhakikisha tunafikia malengo. Sisi tulio kwenye upinzani jicho letu pamoja na kushauri na kupendekeza ni kukosoa pale ambapo walio kwenye Serikali wanakosea. Kukosoa ni tendo la kizalendo na walio Serikalini wawe tayari kukubali kukosolewa ili kuboresha zaidi. Kwa maoni yangu, kama tusipofanya marekebisho ya kimkakati mapinduzi ya Viwanda itakuwa ni nyimbo na ngonjera za kisiasa. Watakaoumia ni Wananchi ambao hawatapata ajira na Serikali yenyewe itakosa kodi kuweza kutoa huduma kwa wananchi. Kama nilivyosema hapo awali Serikali inahitaji kufanya uratibu ili kufikia malengo. Sekta ya Viwanda au Maendeleo ya Viwanda yanapaswa kufungamanishwa na sekta nyengine za uchumi kwa sababu kuna kutegemeana. Kwa Tanzania unahitaji Sekta ya Kilimo inayokua kwa kasi ili kuzalisha malighafi kwenye viwanda. Sekta nyingine kama Elimu, Afya, Nishati, Mazingira nk zinahusiana na Viwanda pia. Kwa leo tutazame Sekta Kilimo na Viwanda kwa muktadha wa Hotuba ya Waziri wa Viwanda na kulinganisha na Hotuba ya Waziri wa Kilimo.
Mheshimiwa Spika, Sekta ya Viwanda na Sekta ya Kilimo kwa pamoja zinachangia nusu ya Pato la Taifa ( GDP) na nusu nyingine ni sekta ya Huduma. Nadharia za Uchumi zinatuambia kuwa Tija ikiongezeka kwenye ya Kilimo inawezesha sekta ya Viwanda kukua na kisha sekta ya Huduma. Hapa Tanzania nan chi nyengine nyingi za Afrika, sekta ya huduma iliruka hatua hizi na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa sana kwenye Pato la Taifa. Ndio maana tuna kitandawili nchini kwetu kuwa Uchumi unakua lakini umasikini haupungui; ni kwa sababu sekta ya huduma haijiri watu wengi kama sekta ya Kilimo na hivyo uchumi unaokuzwa na sekta ya huduma ni nadra kuondoa umasikini. Tanzania bado inapambana na umasikini. Juhudi zote tunazofanya lengo lake ni kuondoa umasikini kwa watu wetu. Sekta za kuondoa umasikini ni Kilimo na Viwanda hivyo lazima mikakati ya Serikali iendane na kufungamanisha haya. Ndio Maana Nchi nyengine Wizara ya Kilimo hujumuisha uongezaji thamani ( Ministry of Agriculture and Agro-processing ). Hatuhitaji kufanya hivyo, tunachohitaji ni kufungamanisha. Hata hivyo Serikali imeshindwa kufanya hivyo katika mwaka wake wa kwanza tu wa Bajeti. Nitaeleza kwa kutumia changamoto tuliyonayo kuhusu Sukari, Mafuta ya Kula na Nguo.
Mheshimiwa Spika, Malengo ya Serikali kwenye Viwanda yapo uk.140 ibara ya 191 ya Hotuba ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Serikali imepanga kutekeleza mambo 9 na katika mambo yote hayo hakuna hata moja linalohusiana na Viwanda vya kuzalisha bidhaa zinazohudumiwa na wananchi wengi zaidi kama Sukari na Mafuta ya kula. Bidhaa hizi ni bidhaa zinazoleta maneno ya kisiasa ndani ya nje ya Bunge. Nadhani baada ya madawa ya kulevya, bidhaa zenye mizengwe mingi zaidi katika duru za kisiasa ni Sukari na Mafuta ya kula. Sukari na Mafuta ya kula imeangusha Mawaziri kadhaa hapa nchini katika kipindi cha miaka 20 iliyopita. Hata hivyo Wizara ya Viwanda na Biashara haina mkakati kabisa kushughulika na Bidhaa hizi licha ya uwezo wake wa kutenegenza ajira na kuokoa fedha za kigeni kuziagiza. Wizara imezungumza kuhusu viwanda vya nguo lakini haijafafanua changamoto kubwa zinazoikabili sekta ya nguo nchini na hasusan biashara haramu ya magendo ya Nguo inayoathiri sana ukuaji wa sekta ya nguo nchini.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, ukitazama hotuba ya Waziri wa Kilimo ambayo Bunge lako tukufu limeshapitisha bajeti yake kuna ‘mikakati’ ya kulima Miwa kwa ajili ya Sukari. Ukurasa wa 44 ibara ya 107 ya Hotuba ya Wizara ya Kilimo na ukurasa wa 25 ibara za 63 na 64 zinaeleza ‘mikakati’ ya kukabiliana na uhaba wa Sukari nchini. Kiambatanisho namba 6 cha Hotuba hiyo kimeeleza kwa kina changamoto nzima ya Sukari na miradi ianyopaswa kutekelezwa ili kumaliza kabisa suala la uhaba wa Sukari nchini. Nimejumlisha miradi ile kutoka kona mbalimbali za nchi na nimekuta ni takribani Hekta 300,000 za kulima Miwa. Kwa Hesabu ya chini ya wastani wa kuzalisha Sukari kwa kila Hekta, miradi hii ikitekelezwa Tanzania itaweza kuzalisha Tani 1.5 milioni za Sukari. Ukiondoa Sukari tunayotumia nchini, ziada itakayouzwa nje inaweza kuliingizia Taifa Fedha za Kigeni USD 500 milioni, sawa na 30% ya malengo ya Mpango wa Maendeleo kwa sekta ya Viwanda katika mapato ya Fedha za kigeni ya USD 3bn. Hapo sijaeleza kiwango cha Ajira kitakachopatikana, ukuaji wa biashara kwenye sekta nyengine na Umeme utakaozalishwa ( Multiplier effect ).
Mheshimiwa Spika, swali la kujiuliza, chukulia Wizara ya Kilimo inalima hiyo miwa hekta 300,000 halafu Wizara ya Viwanda haina mpango wa hivyo viwanda, hii miwa itakwenda wapi? Sio kwamba inapaswa kufungaminisha Kilimo cha Miwa na Viwanda vya Sukari? Ni kwa nini Wizara 2 zilizo chini ya Serikali moja zinashindwa kusomana? Baraza la Mawaziri linajadili nini? Ndio maana Rais anajikuta akitoa matamshi ya Mawaziri barabarani. Suala la Rais kutoa matamko kuhusu Sukari sio sawa, hii ni Kazi ya Mawaziri maana mnam expose Rais. Rais sio mtu wa kuhangaika na masuala ya kunywa Chai na Uji.
Mheshimiwa Spika, nashauri Bunge lako tukufu leo lisipitishe Bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ili Wizara hii ikakae na Wizara ya Kilimo wawianishe mipango hii na kisha walete hapa Bungeni ndio tupitishe.

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.
Featured
Most Popular

Text Widget

Sample Text

Featured

About Me

Followers

TO DARE IS TO DO

TO DARE IS TO DO

OBAMA

OBAMA

INDIAN ICON

INDIAN ICON

Mwalim JK NYERERE

Mwalim JK NYERERE

TANZANIA ICON

TANZANIA ICON

Advertising

Advertising

Facebook

About Us

Ads

Definition List

Pages

Download

Blockquote

Recent Posts

Unordered List

ADVERTISE WITH US @GreatThinkerSays

Popular Posts

Videos